BONDIA MMAREKANI TERENCE “BUD” CRAWFORD AFURAHIA MAPOKEZI TANZANIA, AJIANDAA KUTEMBELEA SERENGETI NA ZANZIBAR – Habari Mpya

Bondia wa kimataifa wa Marekani Terence “Bud” Crawford amesifu ukarimu wa Watanzania tangu alipowasili nchini Mei 24, 2026, kwa ziara ya kitalii. Bondia huyo ameyasema hayo alipokutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi jijini Dar es Salaam akianza ziara yake ya siku kadhaa nchini. Bondia huyo mwenye rekodi ya…

admin Avatar

by

1 minute

Read Time

Bondia wa kimataifa wa Marekani Terence “Bud” Crawford amesifu ukarimu wa Watanzania tangu alipowasili nchini Mei 24, 2026, kwa ziara ya kitalii.

Bondia huyo ameyasema hayo alipokutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi jijini Dar es Salaam akianza ziara yake ya siku kadhaa nchini.

Bondia huyo mwenye rekodi ya kutopoteza pambano lolote katika michezo 42 aliyocheza tangu aingie ndondi za kulipwa, ameeleza pia kusubiri kwa hamu kuona maajabu ya vivutio kama Serengeti, Ngorongoro na Zanzibar atakakotembelea.

Kwa upande wake Dkt. Abbasi kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amemkaribisha nchini na kumwalika kuendelea kuja Tanzania kila atakapohitaji hasa wakati huu ambapo ameamua kustaafu mapema mchezo huo tangu Disemba mwaka jana 2025.

About the Author

About the Author

Easy WordPress Websites Builder: Versatile Demos for Blogs, News, eCommerce and More – One-Click Import, No Coding! 1000+ Ready-made Templates for Stunning Newspaper, Magazine, Blog, and Publishing Websites.

BlockSpare — News, Magazine and Blog Addons for (Gutenberg) Block Editor

Search the Archives

Access over the years of investigative journalism and breaking reports