Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Dkt, Netumbo Nandi-Ndaitwah wakati wakishuhudia utiaji saini wa Hati nne za Makubaliano ya Ushirikiano katika Sekta za biashara, maendeleo ya biashara ndogo na za kati; Ulinzi, pamoja na Ushirikiano wa miji kati ya Manispaa ya Mji wa Zanzibar na Manispaa ya Swakopmund kabla ya kuzungumza na Waandishi wa Habari, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Juni, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Netumbo Nandi-Ndaitwah wameshiriki Jukwaa la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Namibia lililofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam, tarehe 20 Juni, 2026.
















