Mahakama yaifuta kesi ya mgogoro mgawanyo wa rasilimali ya Chadema 

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imeifuta kesi ya madai ya mgawanyo wa rasilimali usio sawa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baina ya Bara na Zanzibar. Kesi hiyo ya madai namba 8323 ya mwaka 2025 ilifunguliwa na Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chadema, Said Issa Mohamed na wajumbe wawili…

admin Avatar

by

1 minute

Read Time

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imeifuta kesi ya madai ya mgawanyo wa rasilimali usio sawa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baina ya Bara na Zanzibar.

Kesi hiyo ya madai namba 8323 ya mwaka 2025 ilifunguliwa na Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chadema, Said Issa Mohamed na wajumbe wawili wa Bodi ya Wadhamini wa Chadema kutoka Zanzibar, Ahmed Rashid Khamis na Maulida Anna Komu (marehemu kwa sasa).

Leo Alhamisi, Mei 28, 2026, Jaji wa Mahakama Kuu, David Ngunyale ameifuta kesi hiyo baada ya kuridhika kuwa hati ya madai ina kasoro kwani haielezi mgogoro huo yaani madai ya ukiukwaji wa sheria katika mgawanyo wa rasilimali uliodaiwa na walalamikaji ulianza lini.

Wadaiwa katika kesi hiyo inayosikilizwa na Jaji Hamidu Mwanga, Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam ni Bodi ya Wadhamini Waliosajiliwa wa Chadema na Katibu Mkuu wa chama hicho.

Endelea kufuatilia Mwananchi

About the Author

About the Author

Easy WordPress Websites Builder: Versatile Demos for Blogs, News, eCommerce and More – One-Click Import, No Coding! 1000+ Ready-made Templates for Stunning Newspaper, Magazine, Blog, and Publishing Websites.

BlockSpare — News, Magazine and Blog Addons for (Gutenberg) Block Editor

Search the Archives

Access over the years of investigative journalism and breaking reports